photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA MAJI TAKA TANGA UWASA, IMEDHAMIRIA KUONGEZA WINGI NA UBORA WA MAJI YANAYOSAMBAZWA NA MAMLAKA HIYO MKOANI HUMO .



MAMLAKA YA MAJI  SAFI NA MAJI TAKA TANGA UWASA, IMEDHAMIRIA KUONGEZA WINGI NA UBORA WA MAJI YANAYOSAMBAZWA NA MAMLAKA HIYO MKOANI HUMO
.
Mamlaka hiyo ambayo hadi sasa imefanikiwa kusambaza maji  safi kwa asilimia 94.5 na kusema kuwa imefanikiwa kupunguza kiwango cha maji taka na kufikiai asilimia 9.4 hadi sasa kwa wateja wa jiji hilo.
Wamesema kuwa hii inatokana na mamlaka hiyo kufahamu umuhimu wa kutoa huduma bora kwa wateja wake sambamba na mikakati iliyojiwekea katika kuhakikisha inaendana na ongezeko la watumiaji wake na kuondoa uhaba wa maji mkoani Tanga.

Imesema hilo litawezekana kwa kuwa tayari imeshaanza ujenzi wa maeneo ya kusafishia maji taka hasa Muheza na Nachingwea,wakati huohuo inaandaa eneo la Utofu lengo likiwa hilo hilo la upatikanaji wa maji safi,jambo litakalo ongeza wingi wa maji safi,wakati huohuo kuondoa kabisa upungufu wa maji, ambapo hadi kufikia sasa mamlaka hiyo inazalisha meta za ujazo 27,740 kwa siku na kukidhi mahitaji ya wateja wake
.
Kuhusu upotevu wa maji, kwa maana ya matumizi yasiyosahihi yanayofanywa na baadhi ya  wateja wake,aidha kwa kutofahamu au kwa makusudi, kupasuka kwa mabomba katika maeneo yaliyokuwa vigumu kuyatambua haraka, mamlaka imesema itahakikisha itaondoa kadhia hiyo, lakini pia itawashirikisha moja kwa moja wananchi,mpaka sasa imefanikiwa kupunguza upotevu huo kutoka asilimia 25.9 hadi asilimia 23
.
Maelezo hayo yametolewa na  mhandisi wa maji mkoani Tanga bwana Chales Alam katika kikao cha baraza la madiwani liliofanyika katika ukumbi wa jiji hilo ambapo mamlaka ya maji safi na maji taka Tanga UWASA na Shirika la umeme Tanzania TANESCO walikuwa waalikwa.

Aidha amesema kuwa hadi sasa mamlaka hiyo imefanikiwa kuwa mamlaka bora Tanzania katika utendaji kwa mwaka 2012/2013 na miaka mingine ya nyuma.

Mbali na mafanikio waliyoyapata lakini pia kuna changamoto mbalimbali zinazochangia kukwamisha baadhi ya malengo kwa mamlaka hiyo kua ni uchakavu wa miundombinu ya maji safi na taka iliyojengwa tangu mwaka 1940,kutegemea chanzo kimoja cha maji cha mto zigi,uchafuzi na uharibifu wa chanzo cha maji kwa watu kuendesha shughuli za kilimo,ukataji miti,uchimbaji wa madini na kadhalika.

Amezitaja changamoto zingine kuwa uharibifu na wizi wa miundo mbinu ikiwemo meta za maji,wateja wasio waaminifu(wizi wa maji),uwezo mdogo kifedha katika kufanikisha miradi ya kuboresha huduma(kutanua na kukarabati miundombinu),chanzo kimoja cha nishati ya umeme kutoka TANESCO, wateja kutolipa kwa wakati ,akitolea mfano taasisi za UMMA.

Amesema ili kuondoa changamoto ya nishati ya umeme mamlaka kushirikiana na benki ya dunia itanunu jenereta kwa ghalama ya shilingi bilioni moja,watabadilisha bomba chakavu katika maeneo mbalimbali yenye urefu wa KM 1,200 hadi 2017,kujenga chemba 15 ili kuongeza uzalishaji wa maji taka,sambamba na kuongeza makusanyo kutoka asilimia 94.5 hadi 99 ya wakazi wa jiji kwa maji safi kutoka 9.4% hadi 9.7% kwa maji taka ifikapo june 2017.

CHALS, amesema mipango ya UWASA kwa sasa ni ukarabati wa majengo,ununuzi wa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa matanki na upanuzi wa huduma, sanjari na uboreshai wa TEHAMA yaani kulipia kwa njia ya simu,itakayosaidia upatikanaji wa huduma kwa haraka na ufanisi,ili hayo yote yaweze kufikiwa  mamlaka inahitaji zaidi ya bilioni 424 katika kipindi cha miaka 3,ambo kwa sasa mamlaka hiyo inakusanya shilingi 7.2bilioni kwa mwaka,lakini wanampango wa kuanza kutumia meter za Pre-paid kwa kuanzia kwa  wateja wachache hasa wateja sugu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment