photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

MKUU wa wilaya ya Lushoto amempa muda wa mwezi mmoja Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lushoto Jumanne Shauri kuhakikisha zahanati ya Migambo inapatiwa huduma umemeAlhaj Majid Mwanga


MKUU wa wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, Alhaj Majid Mwanga amempa muda wa mwezi mmoja Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lushoto Jumanne Shauri kuhakikisha zahanati ya Migambo inapatiwa huduma umeme ndani ya kipindi hicho ili iweze kuwahudumia wagonjwa wakati wote.
Agizo hilo la DC Mwanga limetokana na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara kwenye kijiji cha Migambo ambapo alibaini changamoto kubwa iliyokuwa ikilalamikiwa dhidi ya zahanati hiyo kukosa ni kukosekana kwa nishati hiyo muhimu.
Amesema kimsingi nishati hiyo ni muhimu sana hasa kwenye maeneo ya utoaji huduma hivyo kuamua kutoa agizo hilo ili kuiwezesha zanahati hiyo kufanya kazi zake wakati wote kitendo ambacho kitasaidia kupunguza vifo ambavyo vinaweza kutokana na kukosekana kwa huduma nyakati za usiku.

Amesema ameshangaa kuona zanahati hiyo ikiwa haina nishati wakati nguzo za umeme zimepita karibu na eneo hilo hivyo kutaka suala hilo lishughuliwe ipasavyo lengo likiwa kupatikana ufumbuzi wa changamoto hiyo.

kufuatia hali hiyo,mkuu huyo wa wilaya amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri mbili zilizopo wilayani humo kuhakikisha mikutano yote ya vijiji inafanyika kwa mujibu wa sheria zilizopo ikiwemo kusomwa kwa mapato na matumizi kwa watendaji wa maeneo husika lengo likiwa kurudisha mrejesho kwa wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo yaliyofanyika.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment