photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MJINI MH OMARI R NUNDU , AMEITAKA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA KUHAKIKISHA INAWATENGEA VIJANA NA AKINA MAMA PESA ZA HALMASHAURI

MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MH.OMARI NUNDU
Mbunge wa jimbo la tanga mjini Mh Omari r Nundu , ameitaka halmashauri ya jiji la tanga
kuhakikisha inawatengea vijana na akina mama pesa za halmashauri zilizotakiwa zitengwe kuanzia mwaka 1993 ambapo kwa mkoa wa Tanga zimetolewa miaka mitatu tu, huku miaka18 iliyofuata hazikutolewa au kutokutengwa kabisa.

Mh. Nundu ambae anatumia ahadi ya 4 na 8 za chama cha mapinduzi katika kuliendesha jimbo la tanga amewataka vijana kutokudanganywa kuwa yeye ndie anayezuia mikopo hiyo isitoke badala yake amewataka vijana na akina mama wa mkoa wa tanga kuchangamkia fursa hiyo ambayo ni ya
 kila kijana bila kujali itikadi za vyama.

Aidha Mh.nundu alifika mbali zaidi kwa kuwataka vijana wajijengee kuaminika mara watakapopata mikopo hiyo kwa kuhakikisha wanaitumia kwa malengo.

Itakumbukwa kuwa  Mbunge Omari Rashidi Nundu ,alisamehe mshahara wake wa miaka mitano zaidi ya shilingi milioni 111 kwa kuwakopesha wakazi wa Watanga ili wajikwamue kiuchumi na waondokane na lindi la umasikini uliopo mkoani hapa,pamoja na juhudi hizo,lakini  pesa hizo zilirudi milioni nane tu, na idadi kubwa ya waliokopeshwa wakishindwa kuzirudisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo watu wanaopita wakisema pesa za mbunge huyo zilikuwa za misaada.

Mbunge omar nundu anabaki kuwambunge wa kwanza katika historia ya mkoa wa tanga kusamehe mshaharawake kwa ajili ya kuwakomboa wananchi,amesema pamoja na hayo yote kutokea lakini bado wananchi hao wanafursa ya kukopa,akitolea mfano Benki ya Posta,kwakuwa Benki hiyo kuwa na riba isiyowaumiza wananchi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment