photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

AUAWA KWA KUCHOMWA NA KITU CHENYE NCHA KALI SEHEMU YA TUMBONI, SHINGANO NA KICHWANI MKOANI TANGA.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Fresser Kashai

Mkazi mmoja wa Kijiji cha Mafisa Kata ya Mvungwe Tarafa ya Mgera wilayani Kilindi ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya Tumboni, Shingano na Kichwani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Fresser Kashai amethibitisha kutokea tukio hilo ambalo lilitokea Octoba 7 mwaka huu saa 11:30 wakati Marehemu akiwa shambani kwenye kitongoji baina ya Kijiji cha Mafisa wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda Kashai amemtaja aliyefariki dunia kwenye tukio hilo kuwa ni Lokoye Machaku (29) kabila Mnguu mkazi wa Mafisa wilayani humo ambapo alichomwa kwa kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali kwenye mwili wake.

Aidha amesema kuwa wakati huo mtu mwengine aliyekuwa ameongozana na marehemu Mohamed Mhina (35) mkazi wa eneo hilo alijeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali katika mkono wake wa kulia.

Kamanda Kashai amesema kuwa tukio hilo lilifanywa na watu wawili wa jamii ya wafugaji na walikuwa wamevaa nguo za kimasai na inasadikiwa kuwa ni wakazi wa kijiji cha Lembapuri wilayani Kiteto mkoani Manyara.

Amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kugombania malisho ambapo watuhumiwa walilisha mifugo yao mabua yaliyokuwa shambani baada ya mavuno katika eneo hilo la mafisa.

Hata hiyo amesema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Kilindi kwa ajili ya uchunguzi wakati jeshi hilo linaendelea na msako mkali kuwatafuta wahalifu waliohusika kwenye tukio hilo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment