photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

CHADEMA, NCCR MAGEUZI, CUF NA NLD WAUNGANA LENGO KIKISAMBASATISHA CHAMA CHA MAPINDUZI"CCM"MADARAKANI 2015

CHADEMA, NCCR MAGEUZI, CUF NA NLD WAUNGANA LENGO KIKISAMBASATISHA CHAMA CHA MAPINDUZI"CCM"MADARAKANI 2015....
VYAMA vinne vya upinzani nchini vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), jana vilitiliana saini ya makubaliano ya ushirikiano, ikiwamo kusimamisha mgombea katika chaguzi zote, kuanzia wa serikali za mitaa mwaka huu na ule wa wabunge, madiwani na rais mwaka kesho.

Vyama hivyo ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na National League for Democracy (NLD).

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisoma makubaliano hayo kwa niaba ya makatibu wakuu wa vyama hivyo. Alisema ushirikiano huo watauanza kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, utakaofanyika Desemba 14, mwaka huu.

Alisema kupitia makubaliano hayo, vyama vyote vinne vimekubaliana kuhuisha sera zao na kuchukua yale yanayofanana na kila chama kuyazungumzia hayo kwa wananchi.

"Utaratibu wa namna gani vyama vyetu vitashirikiana katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji mwaka 2014 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 utatolewa katika wakati mwafaka kwa ngazi zote ili waweze kuutumia kama mwongozo wa kufanya kazi,” alisema.

Alisema pia watashirikiana katika mchakato wa kuelimisha umma. kuifahamu na kuipigia kura ya hapana Katiba Inayopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba, ambayo alisema haijazingatia maslahi,wala  maoni ya wananchi.

Alisema vyama hivyo pia vitajenga ushirikiano wa dhati katika mambo yote na hoja zote za kitaifa na zenye maslahi kwa Watanzania.

Aidha, umoja huo uliahidi kulinda Muungano bila kuwa na migongano ya maslahi, kama inavyojidhihirisha katika Katiba Inayopendekezwa.

Slaa alisema pia watahimiza na kusimamia ushirikiano wa pamoja baina ya vyama, asasi na makundi ya Watanzania wenye njia ya dhati ya kulinda na kuenzi muungano bila kunyenyekea maslahi binafsi ya makundi, kabila na itikadi.

Naye, Katibu Mkuu wa CUF na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad alisema Wazanzibar hawaungi mkono katiba hiyo huku Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba akisema katiba hiyo imelenga kuwalinda baadhi ya mafisadi ndani ya CCM.

Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia alisema makubalinao ya vyama hivyo ni kwa maslahi ya taifa na si vyama vyao. Alisema anashangaa kauli za utata zinazotolewa, hivyo kufanya viongozi hao kutoaminika kwa jamii.

Mwenyikiti wa Chadema, Freeman Mbowe alimpongeza Mwenyekiti wa NLD, Emmanuel Makaidi. Pia Mbowe alisema kiongozi au mwanachama yeyote wa Chadema, ambaye atakuwa na lengo la kufifisha juhudi za UKAWA ni vyema akajiondoa, kwa kuwa hawatamvumilia.

Mshikamano baina ya viongozi wa vyama hivyo ulianzia katika Bunge Maalumu la Katiba baada ya kususia vikao, wakidai wanapuuzwa na wenzao wa CCM ambao kimsingi ni wengi katika bunge hilo.

Hata hivyo, wingi wa CCM haukutokana na upendeleo, bali kwa nafasi walizonazo kama wawakilishi wa wananchi.

Wapinzani hao kwa kuungana kwao, wanaamini watakuwa na uwezo wa kukisambaratisha chama tawala cha CCM, katika uchaguzi wa serikali za mitaa, udiwani,ubunge na hata katika nafasi ya Urais hapo mwakani 2014.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment