photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

ROONEY KUWA MFUNGAJI BORA KATIKA RECORD YA TIMU YA TAIFA


Wayne Rooney
Kiungo mshambuliaji wa Manchester United na timu ya taifa ya England Wayne Rooney anajiamini ataweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyeifungia mabao mengi zaidi timu yake ya taifa, England kwa kuvunja rekodi iliyowekwa na Sir Bobby Charlton.

Kwa sasa Rooney anashika nafasi ya nne kwa kuifungia mabao mengi England 41, yakiwa matatu nyuma ya Jimmy Greaves, saba nyuma ya Gary Lineker na nane nyuma ya Charlton mwenye mabao 49.

Kiungo huyo ambaye ana umri wa miaka 28 tu, ndiye Nahodha wa kikosi cha timu hiyo kwa sasa ambacho kitamenyana na San Marino Uwanja wa Wembley usiku wa leo. "Ni wakati wangu sasa kuwapiku wote. Najihisi naweza kabisa kufanya hivyo. Hiyo itakuwa heshima kubwa,"amebainisha
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment