photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

MWALIMU MBARONI KWA TUHUMA YA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA NA MWANAFUNZI WAKE,JE KWA MANTIKI HII BRN ITAFIKIWA,,,?

MWALIMU wa Shule ya Sekondari ya Muungano iliyopo mji mdogo wa Himo wilayani Moshi, Richard Ndoile (30), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, kwa tuhuma za kukutwa gesti na mwanafunzi wake wakifanya mapenzi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita alilieleza gazeti hili jana ofisini kwake, kuwa tukio la kukamatwa kwa mwalimu huyo lilitokea Oktoba 4, saa 5.00 asubuhi, katika gesti ya Kilimanjaro iliyopo Himo.

Moita alisema mwalimu na mwanafunzi huyo (jina limehifadhiwa) ambaye anasoma Shule ya Sekondari Muungano Kidato cha Tatu, walikamatwa baada ya wazazi wa mwanafunzi kumuona binti yao akiwa amepakiwa kwenye pikipiki ya mwalimu wake, kuelekea mahala kusikojulikana.

Alisema hatua hiyo iliwafanya kuhamaki na hivyo kuanza kufuatilia mwelekeo wa pikipiki ili kujua hatma ya safari yao hiyo.

Alisema baada ya kuwafuatilia, pikipiki hiyo ilielekea kwenye gesti hiyo na baada ya kuteremka mtuhumiwa na binti yao waliingia ndani na kuchukuwa chumba, kwa lengo la kutimiza haja zao.

Kwa mujibu wa Kamanda Moita, wazazi waliamua kupiga simu katika Kituo Kidogo cha Polisi cha Himo kwa lengo la kutoa taarifa, ambapo polisi walifika lakini hadi mtuhumiwa anakamatwa tayari walikuwa wameshatekeleza tendo la kujamiiana.

Alisema mwalimu huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kidogo cha Himo, kwa ajili ya kumfikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment