![]() |
| MBUNGE WA KAHAMA JAMES LEMBELI |
Lembeli, mmoja wa wabunge walio mstari wa mbele
katika vita dhidi ya ufisadi, alisema mpango huo ulitekelezwa kwa
kueneza taarifa za kuanzisha jimbo la Ushetu ambalo alitakiwa agombee
badala ya Kahama, lakini baadaye msamaria mwema alimpa taarifa kwamba
jimbo hilo ni halipo.
Lembeli katika mahojiano yake maalumu na gazeti
hili mjini Dodoma alisema alipewa taarifa hizo saa chache kabla ya muda
wa mwisho wa kurudisha fomu za kugombea ubunge na kwamba tukio hilo
lilimfanya afute fomu yake ya kugombea mara mbili.
“Ulikuwa ni uhuni na ufisadi wa hali ya juu
kisiasa,” alisema mwanahabari huyo wa zamani katika mahojiano hayo
maalumu yaliyofanyika mjini Dodoma mapema wiki iliyopita.
Alisema mara ya kwanza alijaza kwamba anagombea
Jimbo la Kahama lakini alifuta na kuandika jimbo la Ushetu baada ya
kupewa taarifa za kuanzishwa kwa jimbo hilo na baadaye alifuta Ushetu na
kuandika tena Kahama baada ya kugundua kuwa ulikuwa mchezo mchafu.
“Baada ya kuruka viunzi, viongozi waandamizi wa
CCM wa Shinyanga, akiwamo Mwenyekiti wa Mkoa, Hamisi Mgeja walisusa
kunifanyia kampeni,” aliongeza Lembeli ambaye aliibuka na ushindi wa
asilimia 54.5 kati ya kura zilizopigwa.
Alisema mpango huo wa kumhujumu ulianza mapema
pale baadhi ya viongozi walipokuwa wakieneza kwamba yeye (Lembeli)
hatakiwi na kwamba ukweli siyo kwamba alikuwa hatakiwi na wananchi bali
baadhi ya viongozi.
Hata hivyo, Makamba alipoulizwa alisema ni uzushi
kwa kuwa kazi ya kugawa majimbo ni ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, CCM
kazi yake ni kusimamisha tu wagombea.
“Niacheni nipumzike niendelee kula pensheni yangu.
Sasa niko Bumbuli natoka kuswali na ninakwenda kula Iddi, niacheni
nipumzike jamani, kama kuna maswali zaidi aulizwe katibu mkuu wa sasa,”
alisema Makamba.
Hata hivyo, Lembeni katika mahojiano hayo
alisisitiza: “Ninachodhani walikaa chini na mambo haya yalifanyika Dar
es Salaam na chakusikitisha zaidi katika ofisi ya Makao Makuu ya CCM kwa sababu
ndio walioleta taarifa.”



0 comments:
Post a Comment