photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema amevutiwa na kasi ya mabadiliko katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA)

wziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Mizengo Kayanza Peter Pinda
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema amevutiwa na kasi ya mabadiliko katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na hasa uanzishwaji wa kozi mpya zinazolenga uongezaji thamani wa mazao ya kilimo (Agri-processing).
 
 Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wahadhiri, wakufunzi, wanafunzi na wanajumuiya ya SUA mara baada ya kutembelea chuo hicho na kukagua utekelezaji wa mradi wa Sayansi na Teknolojia ya Elimu ya Juu (Science and Technology Higher Education Project – STHEP).

Amesema kuwa amefurahishwa na suala la Agri-processing kwa sababu hivi tuna mzigo mkubwa unaoisumbua Serikali nao ni namna ya kununua mazao ya wakulima. 

Ameongeza kuwa Tanzania tuna ziada ya tani milioni 1.5 za mahindi na tani laki nane za mpunga wakati uwezo wa NFRA ni kununua tani 240,000 tu. 

Ameeleza kuwa hayo ni matokeo ya wahitimu waliotoka SUA na kupelekwa wilayani na vijijini wakahimiza kilimo bora kwa wananchi.

Waziri Mkuu ambaye aliwasili Morogoro  akitokea Dodoma, amefanya ziara ya siku kwa kutembelea Chuo Kikuu hicho pamoja na kiwanda cha kutengeneza nguo cha 21stCentury.

Akiwa chuoni hapo, Waziri Mkuu alikagua majengo matatu yaliyojengwa chini ya mradi wa STHEP na kuzindua mawili kati ya hayo, alitembelea maabara za upimaji ubora wa vyakula na kisha kuzungumza na wanaSUA.

 Akizungumza na wanajumuiya hao, Waziri Mkuu aliwataka wawe ni viongozi wa mfano kwa kumiliki walau ekari moja ya shamba, walime au kuweka mifugo ili yale wanayofundisha darasani yaonekane kwa vitendo katika mashamba hayo.

 Mapema,akiwasilisha taarifa ya mradi wa STHEP, Profesa Gerald Monella alisema mradi huo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 7.48 (sawa na sh. milioni 12.5/-) umekisaidia chuo hicho kupata majengo manne yenye kati ya ghorofa moja na mbili, ambayo yameongeza nafasi za kufundishia wanafunzi, vyumba vya maabara na vifaa vyake, kuanzisha mitaala miwili pamoja na kusomesha walimu 21.

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Mama Kate Kamba wakati akitoa salamu za shukrani kwa Waziri Mkuu, amesema Serikali iangalie uwezekano wa kuongeza bajeti ya Chuo kwani kinahitaji fedha zaidi kwa ajili ya kufanya tafiti na kuboresha miundombinu.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment