photo tyyyyyyyyyyyyyyyy_zpsd20272cf.jpg

TATIZO LA ARDHI BADO KUBWA ARUSHA,ASEMA WAZIRI MKUU MSTAAFU EDWARD LOWASA

Ardhi wilayani Monduli mkoani Arusha,Asema LOWASA
WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amesema kuwa tatizo la ardhi wilayani Monduli mkoani Arusha ni kubwa kuliko inavyofikiriwa na umasikini unapiga hodi kwa kasi kubwa katika wilaya hiyo, kutokana na uuzwaji holela wa ardhi kwa thamani ndogo.

Lowassa alisema hayo jana katika semina ya siku mbili ya kutatua tatizo la migogoro ya ardhi iliyokithiri katika wilaya hiyo, semina iliyohusisha viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali ngazi ya wilaya, kata, kijiji na tawi na viongozi wa mila ya jamii ya Kimasai wanaojulikana kwa jina la Laigwanani.

Alisema watu wanaongezeka katika wilaya ya Monduli lakini ardhi kamwe haiwezi kuongezeka lakini Laigwanani kwa kushirikiana na viongozi wa vijiji wanakula rushwa na kuuza ardhi kwa bei ndogo kwa maslahi yao, kitu ambacho ni hatari kubwa kwa wakazi wa Monduli.

Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli na pia alikuwa Mwenyekiti wa semina hiyo, alisema hivi sasa wajane wengi wamekuwa wakidhulumiwa na viongozi wa mila na vijiji kwa kunyang’anywa ardhi na kuwafanya kuhangaika huku na kule bila ya sababu za msingi, na aliwataka viongozi kuacha kufanya hivyo mara moja kwani hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Alisema kibaya zaidi Laigwanani na viongozi wa vijiji wanauza ardhi kwa rushwa kidogo ama kwa kununuliwa kinywaji na kutoa ardhi yenye thamani kubwa kwa bei ndogo, hiyo ni hatari kwa vizazi vijavyo.

Lowassa alisema kuuza ardhi ni sawa na kuuza utajiri na kununua umasikini na kusema kuwa itafika wakati wananchi wa Monduli watakuwa masikini wa kupindukia kwa kufanya maamuzi hayo yasiyokuwa na maana jamii ijayo.

Lowassa alisema enzi za Waziri Mkuu Edward Sokoine, vijiji viliamriwa kutoa ardhi kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya shughuli zao za mafunzo na wafugaji walikuwa wakilisha mifugo yao bila ya shida, lakini kwa sasa kuna wajanja wachache wanataka fidia kwa kitu ambacho hakipo hiyo haitawezekana kamwe.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment